
Baragumu la Mnyonge

![]() |
| Baragumu |
![]() |
| Wahamiaji |
Pamoja
na kwamba mchakato wa kuanza kwa oparesheni ya kuwasaka na kuwatimulia
mbali raia wote wa kigeni wanaoishi nchini kinyume cha sheria
ukiendelea, Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Kagera, kitengo cha Upelelezi,
Doria na Misako kimeanza kuwashughulikia wale wote wanaokwamisha zoezi
la wahamiaji hao kurudi katika nchi zao.
Taarifa
zilizopatikana katika kitengo hicho zinasema kwamba baadhi ya viongozi
wa vitongoji na vijiji wamekuwa wakichukua pesa kwa wahamiaji hao na
kuwaahidi 'kuwalinda' wakati wa oparesheni hivyo wahamiaji hao kuamua
kuahirisha kurudi nchini kwao, Mkuu wa kitengo hicho ASIS. Mwakibinga
amesema tayari baadhi ya viongozi wameshakamatwa na kufikishwa
mahakamani kwa kosa la kuwahifadhi wahamiaji haramu na wengine bado
wanaendelea kusakwa katika oparesheni maalumu iliyopewa jina la 'KAGERA
BILA WAHAMIAJI HARAMU INAWEZEKANA KWA WEWE KUSHIRIKI KIKAMILIFU' — at Bukoba Town
![]() |
| Jivunie Utalii wa Tanzania |



No comments:
Post a Comment