Thursday, 5 September 2013

wahamiaji haramu


Tembo



Kagera. Zaidi ya wahamiaji haramu 45,000 wanaosadikiwa kuishi mkoani humo, bado hawajarejea katika mataifa yao katika kutekeleza agizo la Serikali ya Tanzania la kuwataka kuondoka nchini kwa hiari.
wahamiaji...
Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Kanali mstaafu Fabiani Massawe amesema hayo jana, wakati akiongea na waandishi wa habari kuhusu mchakato wa kufanya msako kuondoa wahamiaji haramu mkoani humo.
Kanali Massawe amesema kufuatia agizo la Serikali ya Tanzania kutaka wahamiaji hao kuondoka kwa hiari, msako wa kuwaondoa kwa nguvu utaanza wakati wowote kuanzia sasa kwa kutumia vyombo vya dola.
Amesema hadi sasa wahamiaji 10,600 ndiyo wameondoka lakini waliojificha maporini na mifugo yao ni wengi ukilinganisha na idadi ya waliotambuliwa.
"Hata hivyo amesema, wanawake waliorejea katika mataifa yao lakini wamezaa watoto na Watanzania hawana budi kurudi katika vijiji walikokuwa ili waume zao wawatafutie vibali waweze kuishi kwa mujibu wa sheria."
Katika maadhimisho ya siku ya mashujaa ,yaliyofanyika kitaifa mkoani Kagera, Rais wa Jamhuri ya Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu,Jakaya Kikwete aliagiza wahamiaji wasio na vibali kurejea katika nchi zao. (Nasib Shabaan).

Kima

No comments:

Post a Comment