Monday, 9 September 2013

TCRA YASISITIZA MAADILI KATIKA UTANGAZAJI

 
 
 
 
BARAGUMU LA MNYONGE


 
Profesa John Nkoma
vyombo vya habari
Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Profesa John Nkoma, amewataka wamiliki wa vyombo vya habari nchini kuendelea kuwakumbusha wafanyakazi wao kufuata maadili ya kazi, ili wasivunje sheria na kanuni ambazo walikubaliana wakati wakikabidhiwa leseni.

Profesa Nkoma aliyasema hayo jijini Dar es Salaam wakati alipokuwa akikabidhi leseni za biashara kwa wamiliki wa Radio Nuuru na Radio Mwambao zilizopo Tanga, Overcomes ya Iringa na Rocks ya Mbeya.

Aidha aliwataka wamiliki wahakikishe wanashirikiana na wafanyakazi wao ili kuepuka uvunjajji wa amani ya nchi ambao unaweza kutokea kwa kutumia vyombo hivyo.
Panya ruwala

No comments:

Post a Comment