Wednesday, 11 September 2013

Zumari ikipulizwa Maziwa Makuu wahemkwao Zanzibar



Simba


Tumeona wiki iliyopita hekaheka ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pale muswada wa  Mabadiliko ya  Sheria ya Katiba, kambi ya upinzani waliposema kwa sauti kubwa wakitetea ushirikishwaji wa wadau hasa kwa upande wa Zanzibar.
Furaha
Zumari
Katika madai yao yale wengi tunayaunga mkono kuwa walikuwa sahihi
kuelezea hisia zao kwamba wadau wa Zanzibar walikuwa na haki ya kusikilizwa mawazo yao, maana sheria inayokusudiwa kutungwa inawahusu pia wao.
Ingawaje zimesomwa barua bungeni kwamba Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) ilishirikishwa,lakini ushiriki huo ni wa upande wa Serikali upande wa wadau ambao tumewasikia siku ya Jumamosi pale katika Hoteli ya Bwawani wakilalamika kutokushirikishwa.
Asasi saba za kiraia hapa Zanzibar zimelalamika kwamba hazijawahi kupata fursa ya  kushirikishwa katika kutoa mawazo juu ya muswada wa sheria hiyo ambao umepitishwa bungeni wiki iliyopita ambao ulizusha malalamiko mengi kutoka kwa kambi ya upinzani ndani ya Bunge.
Taasisi hizo saba ambazo zinaongozwa na Baraza la Katiba Zanzibar chini ya mwenyekiti wake, Profesa Abdul Sharif zilisema Bunge halijawatendea haki kwa kunyimwa fursa ya kutoa mawazo yao katika sheria hiyo.
Asasi hizo saba ziliamua kuitisha mkutano na waandishi wa habari kueleza masikitiko yao. Almasi Mohammed Ali, Katibu wa Zanzibar Youth Forum alikuwa wa kwanza kufungua ukumbi kwa kuwaeleza waandishi wa habari kwamba kushirikishwa SMZ haina maana kwamba wananchi wameshirikishwa.
“Muswada ule ulipokuja mwanzo, viongozi wa Serikali waliitwa Bwawani na sisi raia wa kawaida tuliitwa katika skuli ya Haile Selassie kutoa maoni yetu huu mbona hatujaitwa,” alihoji Katibu Almasi.
Alisema haoni sababu kwa muswada huu wa sheria hiyo kupewa fursa
Kwa Serikali peke yake na wao kama raia wakaonekana kama hawana maana.
“Walijua fika kwamba Wazanzibari hawawezi kukubali kuwa wachache katika Bunge la Katiba na bara kuwa wengi,” anasema Ali.
Mwenyekiti wa Baraza la Katiba Zanzibar,  Profesa Abdul Sharif anasema kwa mujibu wa sheria ingelikuwa vyema  muswada huo ukaonekana katika magazeti ili wananchi watoe maoni yao.


Haki za kiraia ni moja katika mambo ambayo yamelitiliwa mkazo katika Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984. Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  nayo pia imeweka mkazo huo kwa raia.
Uhuru wa kujieleza ni moja ya haki yetu muhimu sana. Ni haki inayoweka msingi kwa uhuru mwingine na heshima ya binadamu ambapo haki ya fikra (right to think) siyo tu kuwa inalindwa kwenye katiba yetu ya sasa, bali hata kwenye mikataba ya Umoja wa Mataifa (UN)na Umoja wa Afrika (AU).Bila shaka tutofautiane katika mawazo, lakini naamini utofauti huo hautaweza kuifanya au kuishawishi Serikali kukataza haki ya fikra kwa kuwa katiba zote mbili zimelinda haki hizo kama zilivyolindwa na mikataba ya kimataifa.
Tunaambiwa kuwa uhuru wa kujieleza ni moja ya haki yetu muhimu hivyo, kuwepo kwa fikra tofauti na mitazamo katika jamii ni sehemu ya kufaidi haki hii ambayo sio hisani kwa raia. Ni haki inayoweka msingi kwa uhuru mwingine na heshima ya binadamu kwa ujumla wake.
Tunaambiwa kuwa uhuru wa kujieleza ni moja ya haki yetu muhimu sana hivyo, kuwepo kwa mawazo tofauti na mitazamo katika jamii ni sehemu ya kufaidi haki hii ambayo sio hisani kwa raia .  Kama wadau Zanzibar wangeshirikishwa nina hakika kilichotokea bungeni kwa kambi ya upinzani kutoka nje wasingefanya hivyo.
Wasingefanya hivyo kwa sababu wasingekuwa na hoja ya kueleza katika suala la ushirikishwaji wa wadau kwa upande wa Zanzibar na hivyo kusingekuwepo kwa hisia ambazo zilielezwa na wengi.
Inaeleweka na kila mmoja wetu kwamba uhuru wa mawazo ni haki inayoweka msingi kwa uhuru mwingine na heshima ya binadamu hapa Zanzibar na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ujumla wake.
Haitawezekana katika jamii wote kuwa na fikra zinazolingana juu ya jambo fulani na kwa maana hiyo ndio kambi ya upinzani walipoona kulikuwa na haja wadau wa Zanzibar nao kutoa mawazo yao ili yaunganishwe pamoja na yale ya wadau wengine.
Ni suala lililo wazi kwamba ustawi wa jamii una uhusiano mkubwa na masuala ya haki za binadamu na kwa sababu hiyo ilikuwa ni haki kwa wadau Zanzibar kutoa mawazo yao katika muswada uliowasilishwa na kupitishwa bungeni. Tunaungana na wabunge waliokosoa suala hilo kule Dodoma, maana kama ingekuwa kwa upande wa Tanzania Bara watu hawakushikirishwa ingekuwa ni sawa, lakini huko wadau wamepatiwa fursa ya kutoa mawazo yao huku hakuna zaidi ya Serikali. Kwa kawaida mwanadamu kukiri upungufu si kitendo cha kujidhoofisha bali ni kitendo cha kujiamini na kujiimarisha. Msimamo wa kujikosoa ni msimamo wa kimapinduzi ambao unazingatia upungufu wa binadamu katika matendo yake ya kila siku, iwe katika siasa, jamii na katika mambo mengine.
Mambo yalivyoanza hadi yalivyofikia tamati ya kupitishwa kwa Muswada ule kila mmoja anafahamu.
Hata hivyo, wadau wa Zanzibar hawatavunjika moyo kutoa mawazo yao katika kuona kwamba tunapata katiba inayotokana na matakwa ya wananchi wenyewe, wataendelea kusema hadi siku ya mwisho.

Utalii

No comments:

Post a Comment