Monday, 23 September 2013

SITTA AONGELEA UMRI WA MGOMBEA URAIS 2015



 
 
MAZINGIRA YETU
 
 
Marais
"LEO NIMEAMKA NIKAWA NA WAZA NANI ATAKUWA RAIS WANGU 2015,JE WEWE MWENZANGU UMESHAMFIKIRIA MTU NISHAWISHI!!!!!"
 
 
 
Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, amesema uzee haupaswi kuwa kigezo cha kumtosa mtu anayetaka kugombea urais 2015, kwa vile fursa hiyo siyo sawa na kutafuta uzuri ‘urembo’ bali kumtafuta kiongozi atakayebadilisha nchi irudi kwenye uadilifu ambao umepotea.

“Kuna suala la kutafuta vigezo ambavyo havina maana, wengine wanazungumzia juu ya ujana na uzee, haya siyo mashindano ya uzuri tunazungumzia kiongozi wa nchi, katika hali ngumu tuliyokuwa nayo kweli unaweza kujaribu urais,” alisema.
Sitta alisema hayo jana wakati akihojiwa katika kipindi cha Medani za Siasa na Uchumi kinachorushwa na kituo cha televisheni cha Star Tv kuhusu siasa za Tanzania.

Alisema wapo wanaosema umri wa kugombea urais upunguzwe uwe miaka 30 na kutolea mfano wa nchi kama Marekani bila kufanya utafiti wa kina katika nchi hiyo.

Sitta alisema nchi kama Marekani inaweza ikaendelea kwa sababu ina taasisi za msingi kama sekta binafsi ambazo zinaingizia serikali fedha hivyo katika nchi hiyo huhitaji rais wa ajabu sababu hata suala la chanjo kwa watoto serikali haihusiki bali limebaki kuwa la sekta binafsi tofauti na hapa kwetu.

“Mwelekeo wangu mtu wa chini ya miaka 40 itakuwa ngumu kuongoza nchi katika hali tulipofikia na kwamba kazi kubwa ni kubadilisha nchi irudi kwenye uadilifu maana tulishajisahau mno tukawaacha viongozi wakafanya biashara wakiwa ndani ya madaraka na sasa ni mabilionea,” alisema.

Sitta ambaye amekuwa akitajwa kuwa miongoni mwa wanasiasa wanaoutamani urais ifikapo mwaka 2015, alisema wakati ukifika yeye kama mwanasiasa atapima upepo kama awanie au la.

Akizungumzia vyama vya upinzani, alisema kwa kiasi fulani vinaendelea kupata nguvu ingawa vingeweza kupata umaarufu zaidi kama vingekuwa vichache kuliko hivi sasa vilivyo vingi.


FUATA NYAYO...
 
 
 
 
 
 
 

No comments:

Post a Comment