MBUNGE AFYATUA RISASI BUNGENI BAADA YA KUTOKEA MABISHANO KATI YAKE NA SPIKA.
MP fires AK-47 during Jordanian parliament session!

Katika hali isiyo ya kawaida mbunge mmoja nchini Jordan alifyatua risasi ndani ya bunge baada ya kutokea mabishano kati yake na mbunge mwenzake ambaye ni Spika wa bunge.
Hata hivyo hakuna mtu aliejeruhiwa na imekuwa ni kawaida kwa Wabunge wa bunge la Jordan kushikana mashati na kurushiana ngumi.
Source: BBC swahili habari saa 3:00 usiku.
A Jordanian MP opened fire on his colleague inside the Jordanian House of Representatives on Tuesday morning, following an argument during the parliamentary session.
According to Roya News, an Amman-based news service, MP Talal Al Sharif opened fire using a Kalashnikov automatic weapon on his colleague MP Qusai Dmeisi the inside of the House of Representatives on Tuesday.
Early reports from Al Ghad news, a Jordanian newspaper, Sharif opened fire using the AK-47 during a Foreign Affairs Council meeting at the House of Representatives, which lies in the Abdali area of Amman.
According to Al Ghad, it was not immediately clear why Sharif opened fire.
Although MP Sharif fired the AK-47, Deputy Qusai Dmeisi (Zarqa, 4th District) was also involved in a brawl in the Parliament earlier this week, when he tried to attack Yihya Saud (Amman, 2nd District) to prevent Saud from accusing Prime Minster Abdullah Ensour. As all parliamentary sessions are filmed, there is a video of the clash between the two MPs from earlier this week.
There is a long history of clashes in the Jordanian parliament, with many sessions having to be adjourned over violence.
CHANZO: http://www.albawaba.com/news/jordan-...ent-gun-519385
Kamati za vyama zinapogeuka
‘kichaka’ cha kuficha wezi
Badala ya kutumika kulinda maslahi ya umma, vikao vya
kamati za vyama vimegeuka kichaka cha kulinda wezi, mafisadi na
wabadhirifu wa mali za umma.
Arusha. Wakati Watanzania
wakitafakari hatima ya Bunge la Jamhuri la Muungano na jinsi
linaloyumbishwa na itikadi za vyama wakati wa uamuzi wa mambo muhimu na
yanayogusa masilahi ya umma, baadhi ya wabunge wanadai bunge hilo
limepoteza sifa.
Wabunge hao kutoka chama tawala, CCM na mpinzani
wake, Chadema wanadai Bunge limepoteza sifa muhimu ya kuwa moja ya
mihimili mikuu ya dola na badala yake limegeuka kamati ya chama.
Katika mahojiano maalumu na gazeti hili jijini
Arusha, wabunge hao, Deo Fulikunjombe, Kangi Lugola, Ally Mohamed
Keissy, wote kutoka CCM na Zitto Kabwe (Chadema), wanakiri kuwa Bunge la
sasa limekosa msimamo wa pamoja katika kusimamia mambo ya msingi
yanayogusa maisha ya wananchi, badala yake mijadala mingi huegemea
itikadi za vyama.
Wakiwa jijini Arusha ambako walihudhuria mkutano
wa kumi wa Umoja wa Kamati za Bunge za Hesabu za Serikali kutoka Nchi za
Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika, SADC (SADCOPAC), wabunge hao
wanadai kuwa badala ya kutumika kulinda masilahi ya umma, vikao vya
kamati za vyama vimegeuka kichaka cha kulinda wezi, mafisadi na
wabadhirifu wa mali za umma.
Kangi Lugola, Mbunge wa Mwibara ameitupia lawama
za moja kwa moja kamati ya CCM inayoongozwa na Waziri Mkuu, Mizengo
Pinda kuwa inawaziba midomo wabunge wa chama hicho tawala kila
zinapoibuka hoja za msingi zenye faida na masilahi kwa umma.
“Wezi, wabadhirifu, mafisadi na watendaji wa
Serikali wanaokiukamaadili na kushindwa kutimiza wajibu wanalindwa
asishughulikiwe na Bunge kupitia kamati ya chama kwa kisingizio cha
kulinda masilahi ya chama na Serikali. Kamati ya chama imekuwa kichaka
cha kulinda wezi?” anasema na kuhoji Lugola.
Anasema Bunge sasa linatumia wingi wa wabunge wa
CCM kama kichaka cha kuridhia kila hoja ya Serikali bungeni bila kupima
faida na madhara yake kwa umma, jambo linalozidi kuwapa sifa wapinzani
ambao licha ya uchache wao, husimama kidete kupinga na hivyo kuungwa
mkono na umma huku CCM ikizidi kupoteza haiba.
“CCM ikitaka kutekeleza ilani yake ya uchaguzi,
basi ituache sisi wabunge wake tuikosoe na kuisimamia Serikali yake
badala ya kazi hiyo kuachiwa upinzani pekee,” anasema na kushauri
Lugola.
Bila kuonyesha mzaha, Lugola anataja mihimili ya
dola iliyosalia sasa baada ya Bunge kupoteza hadhi yake kuwa ni Kamati
za Vyama (Kamati ya Wabunge wa CCM), Mahakama (sheria) na Serikali
(utawala).
Vita dhidi ya ufisadi na dawa za kulevya
Lugola anasema wezi, mafisadi, wabadhirifu wa
fedha na mali za umma pamoja na wafanyabiashara wa dawa za kulevya
nchini wanajulikana kwa majina, sura na mavazi yao, lakini hawaguswi kwa
madai ya kukilinda chama kana kwamba CCM ndiyo inawatuma kutenda maovu
hayo.
“Watu binafsi wanaohusika na uhalifu washughulikiwe kwa maovu
yao wanayoyatenda kwa utashi wao baada ya kukabidhiwa madaraka na ofisi
za umma. Chama kisiwakingie kifua kwa kutuita kwenye kamati,” anasema
Lugola.
Anasema kauli ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri
Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi kuwa akitaja majina ya
wanaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya kutatokea mtafaruku
bungeni, inalenga kudhoofisha hoja na vita ya kupambana na madawa ya
kulevya miongoni mwa wabunge.
“Lukuvi (Waziri) anawatia hofu wabunge ili waogope
kuishinikiza Serikali kutimiza wajibu wake kwa kupambana na janga hili
la dawa za kulevya.
Hakuna shaka kuwa anajenga picha kuwa tunahusika
na tunahonga ili tusikamatwe sisi, ndugu au marafiki zetu wanauza unga.
Serikali haina nia ya dhati kushughulikia wauza unga,” anasema.
Keissy (Mbunge wa Sumbawanga Kaskazini) kwa upande
wake, yeye anakwenda mbele kwa kuitaka Serikali kuwasilisha marekebisho
ya sheria bungeni kuruhusu wezi, mafisadi na wabadhirifu wa fedha na
rasilimali za umma kunyongwa hadharani kama inavyofanyika nchini China
ili kutoa fundisho kwa wengine. “Viongozi wahojiwe utajiri wao wa fedha
na mali nyingi wanazomiliki wao na familia zao mara baada ya kukabidhiwa
ofisi za umma. Wakishindwa washtakiwe, wafungwe maisha na ikiwezekana
wanyongwe,” anasema Keissy
Kwa upande wake, Filikunjombe (Mbunge wa Ludewa)
yeye anawaasa wabunge wenzake bila kujali itikadi zao kuweka mbele
masilahi ya umma badala ya vyama vyao wakati wa kujadili na kuamua hoja
mbalimbali bungeni.
“Ndiyo… vyama vinatupa tiketi ya kugombea. Lakini
tukishakuwa wabunge, hatuongozi wanachama wa vyama vyetu pekee bali
Watanzania wote. Lazima maneno, matendo na uamuzi wetu uweke mbele
masilahi ya taifa badala ya vyama vyetu,” anasema Filikunjombe.
Filikunjombe anaongeza kuwa utashi wa kisiasa
miongoni mwa viongozi ndiyo njia pekee itakayotokomeza wizi, ufisadi,
matumizi mabaya ya fedha na rasilimali za umma pamoja na utoroshaji nje
wa fedha na rasilimali za umma.
Hoja ya wabunge hawa kutoka Tanzania inaungwa
mkono na mwenzao kutoka Uganda ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya PAC
nchini humo, Ssewungu Gonzaga (DP), anayesema vyama tawala barani Afrika
vinaweka mbele itikadi za kisiasa wakati wa kujadili na kuamua hoja
zinazohusiana na wizi, ubadhirifu na matumizi mabaya ya fedha na
rasilimali za umma serikalini.
Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali nchini
(PAC), Zitto Kabwe (Kigoma Kaskazini-Chadema) licha ya kuunga mkono
uwepo na umuhimu wa kamati za vyama bungeni kwa nia ya kulinda nidhamu,
msimamo wa pamoja, itikadi na sera, lakini anasema masilahi ya umma
unapaswa kuwekwa mbele kwenye kila jambo.
“Kamati za vyama zihusike kulinda masilahi ya umma
badala ya vyama. Vyama vya siasa vitakuja na kuondoka lakini taifa na
masilahi ya umma vitadumu milele,” anasema Zitto.
Anawashauri wabunge wote kutumia kwa tahadhari
masilahi yao wakati wa kujadili na kupitisha uamuzi bungeni ili mwishowe
taifa na umma viwe vimenufaika.
Zitto anataja aina tatu za masilahi ya wabunge kuwa ni masilahi
ya taifa, masilahi ya jimbo (wapigakura) na masilahi binafsi (utashi) na
kusema masilahi ya umma yanastahili kuwa juu ya yote.
Mkutano huo wa SADCOPAC uliohudhuriwa na wajumbe
zaidi ya 300 kutoka nchi 28 ulilenga katika kuwajengea wabunge ambao ni
wajumbe wa kamati za hesabu za Serikali uwezo wa kufuatilia na kusimamia
matumizi sahihi ya fedha na rasilimali za umma........
Kuyumba kwa kiti cha spika,
athari zake kwa Bunge
Mpaka sasa kutolewa nje ya ukumbi wa Bunge kwa wabunge
wa upinzani, imeonyesha kuwa uwezo wa kiti cha Spika umefikia mwisho
katika kutafakari uamuzi wake
Tangu kuchaguliwa kwa Spika Anne Makinda na naibu
wake Job Ndugai kuongoza Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kiti
hicho kimeonekana kuwa na changamoto nyingi katika kila kikao cha Bunge
kinachofanyika Dodoma.
Takwimu zinaonyesha mpaka sasa kuna zaidi ya rufaa kumi za malalamiko dhidi ya uongozi na kiti cha Spika.
Rufaa hizo zimefikishwa kwenye uongozi wa kamati
ya kanuni na hadi sasa hakuna hata moja iliyowahi kujadiliwa na kutolewa
uamuzi.
Katika mwendelezo wa matukio ndani ya Bunge hilo,
Septemba 5, mwaka huu, mvutano mkali uliokuwa na dalili mbaya uliibuka
ndani ya Bunge.
Naibu Spika, Job Ndugai alifikia hatua ya kuagiza
Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani, Freemon Mbowe na Mbunge wa Hai
atolewe nje ya ukumbi wa Bunge kwa madai ya ukaidi.
Uamuzi huo ulitolewa baada ya wabunge wote wa
vyama vya CUF, Chadema na NCCR- Mageuzi kusimama na kuendeleza msimamo
wao wa siku moja awali kupinga kuendelea kwa mjadala wa Muswada wa
Sheria wa Mabadiliko ya Katiba na badala wakitaka usitishwe baada ya
kubainika kuwa na udhaifu.
Katika muswada huo, mbali na hoja za Chadema, hoja
kuu nyingine iliyokuwa imeteka Bunge ni kukamilika kwa muswada huo bila
kuwashirikisha Wazanzibari.
Kutokana na mwendelezo wa mivutano hiyo, mitazamo
mbalimbali imekuwa ikijadiliwa huku baadhi wakidai kuwa ni afya na
ukomavu wa Bunge hilo.
Aidha, makundi mengine yamekuwa yakitoa lawama zake kwa viongozi wa kiti hicho, Spika Makinda na msaidizi wake, Ndugai.
Hata hivyo, Ndugai amekuwa akinukuliwa katika
vyombo vya habari akisema kuwa sababu kubwa ya kuwapo kwa vurugu hizo
bungeni ni utovu wa nidhanmu unaoonyeshwa zaidi na wabunge wa kambi ya
upinzani.
Kutokana na mazingira hayo ya Bunge, baadhi ya
wachambuzi wa masuala ya siasa nchini wanaona sababu na mwelekeo wa
Bunge hilo kwa sasa unatupeleka pabaya.
Ukiukwaji wa kanuni
Moja kati ya sababu zinazodaiwa kuwepo kwa
mivutano hiyo ni pamoja na ukiukwaji wa kanuni. Hatua hiyo imekuwa ni
wimbo ndani ya Bunge hilo.
Akizungumza juu ya hilo, Julius Simbeye ambaye
ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu Ardhi jijini Dar es Salaam anasema Spika na
naibu wake wameshindwa kusimamia hata kanuni za Bunge kwa sababu ya
kuendekeza itikadi za vyama.
“Mfano mzuri unakumbuka wakati Bunge la Bajeti ,
mjadala wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Aprili 18 kulikuwa na matusi
yasiyostahili kusikika mbele ya watoto sebuleni, wabunge tusiotarajia
kutukana , mfano Juma Nkamia Peter Serukamba, Mchungaji Peter Msigwa ni
aibu sana,” anasema Simbeye.
Simbeye anasema kutokana na ukiukwaji wa kanuni
unaoruhusiwa na kiti cha Spika, udhaifu unaotokana na mivutano isiyokuwa
na tija imezidi kuongezeka.
“Spika anakosa nguvu, labda ni kwa sababu
ameonekana kutumwa, wanaotukana matusi ni wote, lakini anajikuta
anashindwa kusimamia kanuni na kutumia uamuzi ya kimabavu,”anasema
Simbeye.
Uamuzi ya kimabavu
Mpaka sasa kutolewa nje ya ukumbi wa Bunge kwa
wabunge wa upinzani, imeonyesha kuwa uwezo wa kiti cha Spika umefikia
mwisho katika kutafakari uamuzi wake.
Naibu Spika (Ndugai) ndiye ambaye amekuwa akitumia adhabu hiyo mara kwa mara.
Mfano, katika Bunge la Bajeti alifukuza wabunge wa
Chadema kutohudhuria vikao kwa siku tano. Mbali na hilo wiki iliyopita
aliagiza askari kumtoa nje kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani, Freeman
Mbowe kwa madai ya kuongoza mgomo wa kuendelea na mjadala wa Bunge.
Akisisitiza juu ya hilo, Mkurugenzi wa Taasisi ya
Raia ya kufuatilia Utendaji wa Bunge (CPW),Marcossy Albanie anasema
matumizi ya adhabu hiyo mara nyingi yamekuwa yakitumika kibabe na
kinyume cha kanuni.
“Hakuna kipengele cha kanuni kinachobainisha
ukomo kwa mbunge kuomba taarifa pale anapoona mbunge mwingine
amezungumza jambo lisilokuwa na ukweli, lakini Lissu ametolewa nje
baada ya kuomba taarifa kwa madai ya kuomba mara nyingi, ” anasema
Albanie.
Uwezo wao
Mfanyabiashara wa Mwanza, Merick Masuke anaongeza
kuwa vurugu hizo zinasababishwa pengine na uwezo mdogo wa viongozi hao
katika kukabiliana na hoja za wabunge machachari.
Anasema Bunge la sasa ni tofauti na lile la miaka
10 iliyopita ambapo kuna idadi kubwa ya wabunge wenye uwezo mkubwa wa
kuchambua mambo na wazalendo.
“Ukiangalia uwezo wa wabunge vijana kama vile,
John Mnyika, January Makamba, Zitto Kabwe na wengine wanaonekana kuwa na
uwezo mkubwa wa kujenga hoja zinazomshinda Spika kuzikabili,” anasema
mfanyabiashara huyo.
Kulinda maslahi ya chama.
Sababu nyingine ya vurugu hizo inadaiwa kuwa ni
kutokana na propaganda za kisiasa zilizofanikiwa kuliteka Bunge hilo.
Hatua hiyo imesababisha kuwepo kwa ukandamizaji wa hoja binafsi za
wabunge.
Asasi za Kiraia zikiwamo Kituo cha Sheria na Haki
za Binadamu na The Citizens’ Parliament Watch(CPW), Februari 13 mwaka
huu zilitoa tathmini ya mwenendo wa Bunge hilo ambapo moja kati ya
sababu ilizotaja ni kuzimwa kwa hoja nyingi za wabunge.
Asasi hizo zilieleza kuwa Bunge limekuwa likivunja hoja mbalimbali za wabunge kwa kuangalia maslahi na mitazamo yake.
“Kuna baadhi ya wabunge waliotoa hoja binafsi
zenye maslahi kwa taifa lakini Bunge likazivunja, hiyo siyo haki na
utaratibu wa kibunge lenye kufuata misingi ya kidemokrasia,” ilinukuu
sehemu ya ripoti yake.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa
Gaudence Mpangala anaongeza kuwa hatua hiyo ina mipango ya kujihami na
hatari ya kupoteza nguvu ya chama chake na uaminifu alionao ndani ya
chama na serikali.
“Hatupaswi kuwalaumu Spika na naibu wake wametumwa
tu, kwanza wanahofia yasiwatokee kama ya Samweli Sitta, wanaporuhusu
zaidi hoja za wapinzani ndivyo wanavyozidi kupoteza umaarufu wa CCM. Kwa
hiyo akifuata haki, lazima atakuwa kinyume na CCM, ” anasema Profesa
Mpangala.
Profesa Mpangala anasema uamuzi wa kiti cha Spika umekuwa
ukidhihilisha wazi kutekwa na misimamo ya serikali. Aidha, anasema
kutokana na hoja mbalimbali za kambi ya upinzani, mwonekano huo ni
matokeo ya serikali iliyobakia na chembechembe za utamaduni wa chama
kimoja.
“Kuna sababu za kihistoria, kama kuna maovu na
uchafu utakaoendelea kuibuliwa na upinzani, hali hiyo inaweza kuiathiri
serikali, lakini upinzani wao watakuwa wananufaika. Kwa hivyo mambo haya
yanawajengea wapinzani umaarufu wa kisasa,” anasema ..........
HIVI NI NANI MTETEZI WA WALALAHOI....

No comments:
Post a Comment