Tuesday, 6 August 2013

Agathon Rwasa

 

 

Kiongozi wa chama cha waasi zamani 

nchini Burundi Agathon Rwasa

 kuonekana hadharani leo baada 

ya kipindi cha miaka mitatu 

 

 

 


Add caption
Wafuasi wa Kiongozi wa kihistoria wa kundi la uasi zamani nchini Burundi la FNL, Agathon Rwasa, wanataraji kumuona tena hadharani kiongozi wao leo kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka mitatu baada ya kukimbilia mafichoni.

Kwa mujibu wa Aime Magera msemaji wa kiongozi huyo wa kundi la uasi zamani Agathon Rwasa ambaye aliachana na uasi na kujikita katika siasa na baadaye kurejea katika mafichoni baada ya vurugu zilizoibuka baada ya uchaguzi wa rais wa mwaka 2010 ataonekana hadharani leo.
Aime Magera amewaambia waandishi wa habari kwamba Agathon Rwasa yupo jijini Bujumbura tangu kipindi kadhaa na leo anaonekana hadharani mbele ya halaiki ya wafuasi wa chama chake cha FNL na wageni waalikwa kutoka jamii ya kimataifa.
Msemaji huyo wa Rwasa amethibitisha kuwa kiongozi huyo anakuja kukusanya wafuasi wake na kuwaweka pamoja kwa ajili ya kujiandaa na uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2015 ambapo atawania kiti cha urais.
Juni 2010 Agathon Rwasa alirejea mafichoni kwa kile alichodai anahofia usalama wake. Hata hivyo mauaji ya hapa na pale yalifuatia kutoroka kwa kiongozi huyo aliye vikwa lawama na kundi lake kuhusika katika mauaji hayo.
Serikali ya Burundi ilimchukulia kiongozi huyo kama kiongozi hatari sana kwa usalama wa taifa hilo na kuanzisha harakati za kumsaka bila mafaanikio.

Aime Magera amesema kwamba kiongozi huyo wa upinzani aliachana na uasi na hawezi tena kureja msituni, na kwamba hajawahi kuhamasisha vurugu kama inavyo daiwa. Ameongeza kwamba jamii ya kimataifa imechangia pakubwa katika hatuwa hii.

Duru za kidiplomasia zimethibitisha taarifa hii na kuongeza kuwa juhudi za jamii ya kimataifa zimefaanikisha kumrejesha kiongozi huyo baada ya kukubali kuwa hatoendelea kuukana utawala uliopo.
Tangu mwaka 2010, Agathon Rwasa alitajwa kukimbilia nchini DRCongo katika mkoa wa kivu ya kusini, Tanzania na Zambia, lakini msemaji wake amesema kiongozi huyo hajawahi kutoka katika ardhi ya Burundi, na alikuwa akijificha miongoni mwa wananchi ambao walimuhudumia kwa kipindi chote hiki.

No comments:

Post a Comment