SPIKA MAKINDA AWATAKA WABUNGE KUTOPOKEA RUSHWA
SPIKA MAKINDA AWATAKA WABUNGE
SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Anne Makinda
(MB), amewataka wajumbe wa kamati za Bunge kuachana na tabia ya kupokea
bahasha (rushwa) kwa kuwa itachangia kuiuza nchi.
Akizungumza
wakati wa kufungua mafunzo ya wajumbe wa kamati tatu za Bunge za
Serikali za Mitaa (LAAC), Hesabu za Serikali (PAC) na ile ya Bajeti,
Makinda alisema kuwa ni vyema wajumbe wa kamati hizo wakatumia nafasi
waliyokabidhiwa kwa ajili ya kutoa huduma za msingi kwa wananchi.
Alisema kuwa iwapo wabunge watashindwa kuwa waadilifu na badala yake
wakaendelea kupokea bahasha hizo kuna hatari ya kuiuza nchi na hivyo
kutaka tabia hiyo ikome mara moja.
“Iwapo sisi wabunge katika
kamati zetu hatuwi waadilifu, ndugu zangu tutakuwa tunaiuza nchi hii,
naomba bahasha, tafadhali, zikome mara moja kwa upande wetu,” alisema.
Akitolea mfano, Makinda alisema kuwa Bunge la Uingereza liliwachukulia
hatua kwa kuwafungulia kesi za jinai wabunge wake waliobainika kupokea
mapato ya udanganyifu/ ziada.
Spika Makinda alisema kuwa ni
vyema wabunge wakatunza maadili yao kwa kuwa masuala kama hayo yanaweza
kutokea, kwamba wakionyesha mfano mzuri hata wanaotoa bahasha wataogopa
na kuweka hesabu zao vizuri.
No comments:
Post a Comment