DR. MWAKYEMBE : AWASHUKIA WANAOWASAIDIA WAUZA UNGA
DR. MWAKYEMBE : AWASHUKIA
WANAOWASAIDIA WAUZA UNGA
 |
| Madawa ya kukevya |
WAZIRI wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe, amewataka watendaji wa
Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini (TAA), kuachia ngazi endapo dawa za
kulevya zitavushwa kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu
Nyerere (JNIA) bila wao kujua.
Waziri huyo aliyasema hayo
wakati akizindua kamati ya nne ya kitaifa ya usalama wa usafiri wa anga,
katika ukumbi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) jijini Dar
es Salaam.
Mwakyembe ambaye aligoma
kusoma hotuba yake aliyoandaliwa kwa ajili ya uzinduzi huo, alisisitiza
kuwa endapo tukio kama hilo litatokea tena ni bora watendaji hao
wakajiweka tayari kujiondoa mapema kabla hajawafikia.
Dk.
Mwakyembe amesema ni aibu na jambo la kushangaza kuona dawa zinavushwa
wakati watendaji hao wapo, hivyo akawataka kujiwajibisha kwanza kabla ya
hatua nyingine kufuata dhidi yao.
Alisema suala la ulinzi na
usalama katika viwanja vyetu ni fedheha na kashfa kubwa iliyoikumba nchi
kutokana na kupitishwa kirahisi kwa dawa za kulevya kwenye JNIA, ambao
unabeba jina la Baba yetu wa Taifa.
“Tusitafute visingizio katika hili, huu ni udhaifu mkubwa ambao umetuletea ‘udhaifu’ mkubwa kitaifa,” alisema.

No comments:
Post a Comment