Kutoka IKULU:Rais Jakaya Kikwete Akutana na Vijana Walioachana na Matumizi ya Dawa za Kulevya IKULU Jijini Dar es Salaam


Kijana
Jimmy Changchuu alieachana na matumizi ya dawa za kulevya akimkabidhi
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete picha aliyochora yeye na kijana mwenzake
wakati vijana hao walimpomtembelea Rais Ikulu jijini Dar es Salaam
leo.Vijana hao wanalelewa katika kituo cha Pilli Missanah Foundation
kilichopo Kigamboni Jijini Dar es Salaam.

Vijana
walioachana na Matumizi ya dawa za kulevya kutoka katika kituo cha
Pilli Missanah Foundation kilichopo Kigamboni jijini Dar es Salaam
wakiwa katika picha ya pamoja na Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete ikulu
jijini Dar es Salaam leo.Kulia pembeni ya Rais ni Mwanzilish Kituo hicho
Bi.Pilli Missanah na watatu kushoto ni mfadhili mkuu wa kituo hicho
Bwana Zacharia Hans Poppe.Picha na Freddy Maro-IKULU
----
Rais Jakaya Mrisho
Kikwete ameiagiza Wizara ya Afya kupitia kitengo cha magonjwa ya
akili pamoja na Tume ya Kuratibu Udhibiti wa Dawa za Kulevya nchini
kushirikiana na Kituo cha Ushauri Nasaha cha Pili Misana Foundation,
ambacho kinawasaidia waathirika wa madawa ya kulevya ili kiweze
kuwahudumia watu wengi zaidi hapa nchini.
Rais Kikwete amesema hayo leo Ikulu alipokutana na vijana walioachana na matumizi ya dawa za kulevya ambao wamepata ushauri nasaha na usaidizi kutoka katika kituo cha Pili Misana kilichopo Kigamboni jijini Dar es Salaam.“Jamii lazima ishiriki katika utatuzi wa jambo hili, ni tatizo kubwa na linamgusa kila mtu na inabidi wote tushiriki katika kulipiga vita” Mhe. Rais amesema na kumpongeza Bi. Pili Misana na
Rais Kikwete amesema hayo leo Ikulu alipokutana na vijana walioachana na matumizi ya dawa za kulevya ambao wamepata ushauri nasaha na usaidizi kutoka katika kituo cha Pili Misana kilichopo Kigamboni jijini Dar es Salaam.“Jamii lazima ishiriki katika utatuzi wa jambo hili, ni tatizo kubwa na linamgusa kila mtu na inabidi wote tushiriki katika kulipiga vita” Mhe. Rais amesema na kumpongeza Bi. Pili Misana na
Zacharia Hans
Pope ambaye ndiye mfadhili wa kituo hicho ambacho tayari vijana wapatao
203 wamepatiwa huduma ya ushauri nasaha na kuweza kuachana na madawa ya
kulevya na kurudia katika shughuli zao za kimaendeleo.
Rais Kikwete amesema tatizo la madawa ya kulevya ni la muda mrefu lakini hapo awali lilikuwa halisikiki sana kwa sababu jitihada za kuzuia madawa hayo zilikua hazitangazwi wala kufuatiliwa sana.“Sasa hivi juhudi mbalimbali za kupambana na madawa ya kulevya zinatangazwa na hivyo kusikika sana na pia taarifa nyingi zinazohusiana na madawa ya kulevya zinawekwa wazi kwa jamii” Mhe. Rais amesema na kueleza kuwa taarifa nyingi zinawekwa wazi na kutangazwa ili kushirikisha jamii katika kupambana na tatizo hili.
Kiasi cha vijana 35 leo wamefika Ikulu ambapo wametoka katika nyanja mbalimbali za kitaaluma, elimu na kijamii na pia umri tofauti kutoka miaka 14 hadi miaka 53. Kituo hicho kinahudumia watu wenye jinsia tofauti wake kwa waume kutoka sehemu mbalimbali nchini.
Rais Kikwete amesema Serikali inafanya jitihada kubwa sana za kuwasaidia vijana mbalimbali na bado itaendelea kutoa msaada huo, huku juhudi mbalimbali za kupambana na madawa hayo zikiendelea.
Naye mfadhili wa kituo hicho Bw. Zacharia Hans Pope ameitaka jamii kushiriki na kuwa karibu zaidi na vijana ili kuweza kusaidia katika mapambano ya madawa ya kulevya na athari zake nchini.
Imetolewa na;
Rais Kikwete amesema tatizo la madawa ya kulevya ni la muda mrefu lakini hapo awali lilikuwa halisikiki sana kwa sababu jitihada za kuzuia madawa hayo zilikua hazitangazwi wala kufuatiliwa sana.“Sasa hivi juhudi mbalimbali za kupambana na madawa ya kulevya zinatangazwa na hivyo kusikika sana na pia taarifa nyingi zinazohusiana na madawa ya kulevya zinawekwa wazi kwa jamii” Mhe. Rais amesema na kueleza kuwa taarifa nyingi zinawekwa wazi na kutangazwa ili kushirikisha jamii katika kupambana na tatizo hili.
Kiasi cha vijana 35 leo wamefika Ikulu ambapo wametoka katika nyanja mbalimbali za kitaaluma, elimu na kijamii na pia umri tofauti kutoka miaka 14 hadi miaka 53. Kituo hicho kinahudumia watu wenye jinsia tofauti wake kwa waume kutoka sehemu mbalimbali nchini.
Rais Kikwete amesema Serikali inafanya jitihada kubwa sana za kuwasaidia vijana mbalimbali na bado itaendelea kutoa msaada huo, huku juhudi mbalimbali za kupambana na madawa hayo zikiendelea.
Naye mfadhili wa kituo hicho Bw. Zacharia Hans Pope ameitaka jamii kushiriki na kuwa karibu zaidi na vijana ili kuweza kusaidia katika mapambano ya madawa ya kulevya na athari zake nchini.
Imetolewa na;

No comments:
Post a Comment