Sunday, 11 August 2013

Ni sisi wana Jambo Bukoba.


 
 JAMBO BUKOBA

 
 
 
Wapendwa marafiki wa Jambo Bukoba,

Tunafurahi kuwajulisha kuwa jana tumewapokea Luka na Tine kutoka Ujerumani ambao tutakuwa nao kwa mwaka mmoja. Tunamshukuru Mungu wamefika salama wakitokea Dar es salaam kwa basi hadi Bukoba. Tunawakaribisha sana katika kikosi kazi chetu cha Jambo Bukoba.

Ijumaa Gonzaga alikwenda Karagwe kwa ajili ya kuanza shughuli ya ujenzi wa chumba cha darasa Karalo Shule ya Msingi. Jumatatu hadi ijumaa tutakuwa Muleba kwa ajili ya semina ya walimu wa michezo. Tutakuwa na mwalimu Sweetbert toka Katebenga shule ya msingi kama mwezeshaji. Tutatumia muda huo pia kusaini mkataba wetu na viongozi wa Halmashauri ili kutengeneza madawati sistini ya shule ya msingi Kishoju.

Siku ya Alhamisi tulikwenda nane nane katika uwanja wa Kyakailabwa. Huko tulifurahi sana kujumuika na marafiki, kula na kunywa na kuona mazao mbali mbali ya wakulima.

Tunawatakia wikendi njema.

Ni sisi wana Jambo Bukoba.Wapendwa marafiki wa Jambo Bukoba,

Tunafurahi kuwajulisha kuwa jana tumewapokea Luka na Tine kutoka Ujerumani ambao tutakuwa nao kwa mwaka mmoja. Tunamshukuru Mungu wamefika salama wakitokea Dar es salaam kwa basi hadi Bukoba. Tunawakaribisha sana katika kikosi kazi chetu cha Jambo Bukoba.

Ijumaa Gonzaga alikwenda Karagwe kwa ajili ya kuanza shughuli ya ujenzi wa chumba cha darasa Karalo Shule ya Msingi. Jumatatu hadi ijumaa tutakuwa Muleba kwa ajili ya semina ya walimu wa michezo. Tutakuwa na mwalimu Sweetbert toka Katebenga shule ya msingi kama mwezeshaji. Tutatumia muda huo pia kusaini mkataba wetu na viongozi wa Halmashauri ili kutengeneza madawati sistini ya shule ya msingi Kishoju.

Siku ya Alhamisi tulikwenda nane nane katika uwanja wa Kyakailabwa. Huko tulifurahi sana kujumuika na marafiki, kula na kunywa na kuona mazao mbali mbali ya wakulima.

Tunawatakia wikendi njema.
Ni sisi wana Jambo Bukoba.

No comments:

Post a Comment