Wednesday, 21 August 2013

MSAFARA WA MBIO ZA MWENGE WAPATA AJALI

 
 
 
MSAFARA WA MBIO ZA 
MWENGE WAPATA AJALI


Magari matano yaliyokuwa katika msafara wa kukimbiza Mwenge wa Uhuru yalipata ajali jana katika kijiji cha Fufu kilichoko wilayani Chamwino. Magari hayo yalikuwa yakitokea Wilaya ya Dodoma kuelekea kwenye makabidhiano wilaya ya Mpwapwa.

Katika ajali hiyo watu tisa wakiwemo kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru, Juma Ally (32) wamejeruhiwa na kulazwa katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma. KWa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Dodoma ni kwamba hali za majeruhi zinaendelea vizuri.

Ajali hiyo ilisababishwa dereva wa moja kati ya magari ya msafara , kushika breki ghafla baada ya kukutana na tuta na kusababisha magari yaliyokuwa nyuma yake kugonga gari la mbele yake. KWa kiasi kikubwa hali hii ilisababishwa na vumbi kubwa lililotokana na ujenzi unaoendelea wa barabara ya kutoka Dodoma – Iringa.

 
(Pichani : Polisi wakikagua moja ya magari
 yaliyogongana katika ajali hiyo)
 
 

No comments:

Post a Comment