Saturday, 31 August 2013

KIKOSI KAZI CHA UHAMIAJI...

BARAGUMU LA MNYONGE
 
Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Kagera imeanza kampeni ya kuwahamasisha wahamiaji haramu ambapo mpaka sasa hawajaondoka nchini kurudi makwao kuomdoka mara moja kabla ya kuanza kwa zoezi la kuwaondoa kwa nguvu katika oparesheni inayotarajiwa kuanza wakati wowote kuanzia sasa.

Mfawidhi wa kitengo cha Upelelezi, Doria na Misako katika idara hiyo mkoa wa Kagera ASIS. Jeremiah Mwakibinga
Mmoja wa Maofisa uhamiaji akifuatilia kwa makini maelezo yaliyokuwa yakitolewa na ASIS. Mwakibinga wakati akiongea na viongozi na wananchi wa kijiji cha Ruhama
alisema kwamba kwa kuanza kampeni hiyo imeanza katika wilaya ya Bukoba Vijijini na baadaye itaendelea kwa wilaya zote za mkoa wa Kagera.
ASIS. Mwakibinga, ambaye ni Mkuu wa Kitengo cha Upelelezi Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Kagera akisikiliza swali kutoka kwa mmoja wa wananchi katika kijiji cha Ruhama alipokwenda kuhamasisha wananchi na viongozi kushirikiana na Idara hiyo kuwataka wahamiaji haramu kuondoka nchini kwa hiyari

Alisema kwamba kampeni hiyo imelenga si kwa wahamiaji pekee bali pia kwa viongozi na wananchi kwa ujumla. ''Tunajua kwamba Wahamiaji Haramu wakituona wanakimbia, mfano tulipofika katika kijiji cha Kagarama, hivyo kampeni hii tunaifanya kwa viongozi wa vijiji na wananchi pia. Tumeongea na wananchi
Kikosi cha Upelelezi chini ya Kamanda Mwakibinga wakiongea na Afisa Mtendaji wa kijiji cha Katerero
katika vijiji vya Kibirizi, Rugazi, Kagarama, Masheshe na Katoro kwamba wao washirikiane nasi kwa kuwakataa wahamiaji haramu kwani wanajua na wanaishi nao siku zote, kuwakataa manake kuwaeleza ukweli kwamba warudi kwao, pia wananchi wawashinikize viongozi wao kuwaondoa wahamiaji haramu. Kwa upande wa viongozi wa vijiji na kata, tumewasisitiza kwamba wafanye juhudi katika kuwahimiza wahamiaji hawa waondoke, na kama mtu kaambiwa aondoke halafu amekataa basi walete taarifa ofisini kwetu siye tutamshughulikia.'' Alieleza Mwakibinga.

Wahamiaji haramu kutoka nchi za Rwanda, Burundi na Uganda ambao wapo katika mkoa wa Kagera inasemekana waliondoka na sasa wameanza kurejea tena nchini baada ya kuona kuwa Oparesheni aliyosema Raisi wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dokta Jakaya Mrisho Kikwete ya
Maafisa Uhamiaji wakiranda mitaani katika kijiji cha Masheshe wilaya ya Bukoba Vijijini
kuwaondoa kwa nguvu wahamiaji haramu baada ya wiki mbili haifanyiki, wengi wamerudi wakidai ile ilikuwa ni 'danganya toto' tu hakuna oparesheni itakayokuja.



 


Wananchi wa kijiji cha Kibirizi wakimsikiliza Kamanda wa Upelelezi Uhamiaji mkoa Kagera wakati alipokuwa akiongea nao kuhusu suala la wahamiaji haramu mkoa wa Kagera

No comments:

Post a Comment